Merz atangaza baadhi ya mawaziri wa serikali ijayo
29 Aprili 2025Matangazo
Mshirika wa karibu wa Merz Johann Wadephul anatarajiwa kuwa waziri mpya wa mambo ya nje, aliyewahi kuwa mkuu wa sekta ya nishati Katherina Reiche atakuwa waziri wa uchumi, Alexander Dobrindt ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani.
Soma pia: Merz akaribia kushika usukani wa kuiongoza Ujerumani
Chama cha SPD ambacho jana kiliidhinisha makubaliano na CDU ya kuunda serikali ya mseto, kinatarajiwa wiki hii kutangaza majina ya mawaziri wake, lakini Boris Pistorius wa SPD anatarajiwa kusalia katika nafasi yake ya waziri wa ulinzi. Hata hivyo Bunge linatakiwa kumchagua rasmi Merz kama Kansela mpya wa Ujerumani.