Merz aionya Ujerumani kuwa makini katika usalama
28 Juni 2025Matangazo
Akiwa katika ziara rasmi ya Makao Makuu ya Kamandi ya Operesheni za Kijeshi za Bundeswehr, karibu na mji wa Potsdam, Merz alieleza kuwa hali ya sasa ya kiusalama duniani, hususan vita vya Urusi dhidi ya Ukraine, inatoa ujumbe wa wazi kwa Ujerumani na washirika wake.
Ziara hiyo ilifanyika ikiwa ni sehemu ya Siku ya Majeshi ambapo vikosi vya ulinzi hujitambulisha kwa wananchi katika maeneo 10 tofauti. Aidha Merz alitumia fursa hiyo kuwashukuru wanajeshi kwa huduma yao kwa taifa.