Mazungumzo ya Urusi na Marekani ya nyuklia hayaridhishi
10 Februari 2025Matangazo
Ikitoa maoni yake mwezi uliopita, baada ya rais wa Marekani Donald Trump kusema anataka kupunguza matumizi ya silaha za nyuklia, ikulu ya Kremlin ilisema kuwa Rais wa nchi hiyo Vladimir Putin aliweka wazi kwamba anataka kuanzisha tena mazungumzo ya kupunguza silaha za nyuklia haraka iwezekanavyo.
Lakini Ryabkov amesema kuwa Marekani inataka mazungumzo ya pande tatu yanayoijumuisha China huku Urusi nayo inataka mazungumzo ya pande tano.
Urusi imesema inaitaka Uingereza na Ufaransa pia kushirikishwa katika mazungumzo yoyote mapya ya udhibiti wa silaha hizo za nyuklia.