Mazungumzo ya nyuklia Geneva yamalizika bila mafanikio
27 Agosti 2025Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Iran, Ismail Baghaei, ameliambia shirika la habari la nchini humo kwamba, wahusika walibadilishana maoni katika mkutano huo wa Geneva.
Lakini bila ya kufikia makubaliano mwishoni mwa mwezi Juni, juu ya mpango wa nyuklia waIran, kati ya taifa hilo na mataifa hayo matatu ya Ulaya, Jamhuri hiyo ya Kiislamu iko katika hatari ya kurejeshewa vikwazo ilivyowekewa na Umoja wa Mataifa ifikapo mwishoni mwa mwezi Agosti.
Nchi za Ulaya kujadili na Iran kuhusu mpango wa Nyuklia
Awali mataifa hayo yanayojulikana kama E3 yalikutana na wajumbe wa Iran mjini Istanbul kwa lengo la kuishinikiza serikali kufikia makubaliano ya kidiplomasia. Mazungumzo hayo yalikuwa ya kwanza tangu Israel na Marekani walipoishambulia Iran katikati ya mwezi Juni.