Mazungumzo ya amani Gaza yatatizwa na misimamo ya Israel
12 Julai 2025Matangazo
Vyanzo hivyo vimesema kuwa mazungumzo ya Doha yanakabiliwa na vikwazo na changamoto nyingi kutokana na msisitizo wa Israel, kufikia jana Ijumaa, wa kuwasilisha utaratibu wa kujiondoa katika eneo hilo, ambalo kimsingi unaonyesha kujipanga upya kwa jeshi hilo katika eneo hilo badala ya kujiondoa.
Mazungumzo ya amani Gaza yapiga hatua muhimu- Doha
Hamas imesema inataka kuondolewa kikamilifu kwa wanajeshi wa Israel kutoka Gaza, ambayo ni makazi ya zaidi ya watu milioni mbili.
Vyanzo hivyo vimeongeza kuwa wapatanishi katika mazungumzo hayo, wamezitaka pande zote mbili kuahirisha mazungumzo hayo hadi atakapowasili mjumbe maalum wa Rais wa Marekani Donald Trump, Steve Witkoff, mjini Doha.