SiasaUbelgiji
Mawaziri wa NATO wajadili mustakabali wa Ukraine
4 Aprili 2025Matangazo
Katika mkutano huo, mawaziri wa mambo ya nje wa Ulaya wameilaumu Urusi kwa kuzuia msukumo wa Marekani wa kuleta amani na kutoa wito wa kuiwekea shinikizo kali Moscow kukubali kusitisha mapigano.
Soma pia:Wanachama wa NATO waahidi kuongeza matumizi yao ya ulinzi
Kwa mujibu wa vyanzo, Ikulu ya White House inatilia mashaka nia ya Rais wa Urusi Vlamir Putin katika siku za hivi karibuni, ingawa Rais Donald Trump anaendelea kuashiria hadharani imani yake kwamba Putin anataka kumaliza vita.
Soma pia:Rutte: Marekani itandelea kuiunga mkono NATO
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noël Barrot amesema Moscow inapaswa kutoa jibu kwa Marekani ambayo inafanya kila juhudi katika kufanikisha usitiswaji mapigano.