Katika matangazo yetu ya jioni: Sintofahamu yatanda baada ya kutokea tetemeko la ardhi Korea Kaskazini. Tetemeko jipya lakumba Mexico. Merkel na Schulz wawasihi wapiga kura wasikichague chama cha AfD katika uchaguzi utakaofanyika hapo kesho tarehe 24 Septemb. Polisi wa jimbo la Puntland wakamata mashua iliyosheheni silaha kutoka Yemen.