Mataifa ya Kiarabu yasaka njia dhidi ya mipango ya Trump
22 Februari 2025Shirika la habari la serikali ya Saudi Arabia, SPA limeripoti hayo.
Nchi za Kiarabu zinapambana kusaka mpango mbadala wa ule uliopendekezwa na Rais wa Marekani Donald Trump wa kuibadilisha Gaza na kuwahamishia watu wa Gaza kwenye mataifa jirani ya kiarabu.
Mkutano huo ulioitishwa na Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman, alihudhuriwa na Mfalme Abdullah wa Jordan, Emir wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al-Thani, Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan, Emir wa Kuwait Sheikh Meshal al-Ahmad al-Sabah na Mwanamfalme wa Bahrain Salman bin Hamad Al-Khalifa.
Vyanzo vinavyofahamu mazungumzo hayo viliiambia Reuters kwamba wakuu hao walililishughulikia pendekezo la Misri, ambalo huenda likajumuisha dola bilioni 20 za ufadhili kwa zaidi ya miaka mitatu.