Sheria na HakiMashariki ya Kati
Mashirika ya misaada Palestina yakosoa sheria mpya za Israel
17 Machi 2025Matangazo
Wafanyakazi hao wanaoyahudumia maeneo ya Gaza na Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu wamezitupia lawama mamlaka za Israel kwa kuweka sheria kali na vikwazo mbalimbali ambavyo vinafanya kazi zao kutotekelezeka.
Soma pia:Mashirika ya Misaada Palestina yazihofia sheria mpya za Israel
Mashirika ya misaada yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi katika maeneo ya Palestina tayari yanakabiliwa na matatizo mengi. Takriban wafanyakazi 387 wameuawa huko Gaza tangu kuanza kwa vita.