MigogoroMashariki ya Kati
Wapalestina wengine 15 wauawa Ukanda wa Gaza
4 Julai 2025Matangazo
Hayo yanaripotiwa wakati Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ikieleza kuwa watu 613 wameuawa karibu na misafara ya kiutu na maeneo yanayotumiwa kugawa chakula, tangu jeshi la Israel lilipoanza operesheni zake Gaza mwishoni mwa mwezi Mei.
Msemaji wa ofisi hiyo Ravina Shamdasani amesema ni wazi kuwa jeshi la Israel liliwashambulia Wapalestina waliokuwa wakijaribu kufikia vituo vya kugawa msaada vilivyo chini ya taasisi ya kiutu ya Gaza.