MigogoroMashariki ya Kati
Watu 82 wauawa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel
3 Julai 2025Matangazo
Hayo yameelezwa na mamlaka za hospitali pamoja na Wizara ya Afya na kuongeza kuwa watu wengine watano waliuawa karibu na wakfu wa kutoa misaada wa GHF unaoungwa mkono Israel na Marekani na ambao umekuwa ukikosolewa kwa namna unavyoendesha shughuli zake kwa kuhatarisha maisha ya raia wenye uhitaji.
Hadi sasa mazungumzo yanayolenga usitishwaji mapigano huko Gaza yanaendelea huku rais Donald Trump wa Marekani akisema kuwa mpango wa kusitisha mapigano kwa siku 60 unakaribia kufikiwa baada ya Israel kukubali vipengele muhimu vya makubaliano hayo. Hata hivyo Hamas hawajatoa jibu lao la moja kwa moja.